Wednesday 22 December 2010

NIIKUMBUKAVYO MIMI DESEMBA 23, 1999.

Picha ya ajali

Ikiwa mida ya saa kumi na moja jioni, tukiwa nyumbani kijijini (NYAKIBALE) Baba aliniita na kunituma kwa Baba mkubwa katika kijiji cha jirani. Nikiwa huko mala nikapata tetesi kuwa kaka yetu mkubwa Mubelwa T, aliyekuwa safarini kutokea Dar kuja nyumbani Bukoba kapata ajali. Katika kupeleka ujumbe kwa Baba pia nikajikuta nikilieleza hili ndipo kuulizwa  kapatia wapi hiyo ajali na kusema sijasikia ni wapi kwani sikulichukulia suala la ajali kama jambo zito kutokana labda na kutokujua ajali ilikua ni nini kwa wakati huo. Nikaagizwa tena kwenda uliza hiyo ajali imetokea wapi?
Nilienda mbio bila kujali kama ni kweli ila nikihisi ni ile hali ya undugu ndio ilikua ikinisukuma kufanya yale yote na nilipofika nikaelezwa kuwa imetokea maeneo yaitwayo IGOMBE takribani kama kilometa 30 kutoka nyumbani tulipokuwa.
Ikumbukwe kwamba hiki kilikua ni kipindi cha maandalizi ya sikukuu za Krisimas na Mwaka mpya hivyo kila jambo lililohusiana na ajali hata leo huwa haliombewi ili ndugu, jamaa, wapenzi na hata wazazi wetu wasafiri na kufika na kusherehekea salama kwa pamoja huku wakifurahi, hivyo kupeleka taarifa ile ilileta hisia sana kwa wote hasa wazazi waliojua kabisa maneno yaliyosemwa na mototo kama mimi (kwa kipindi hicho) hayakua ya kujitungia.
Ilibidi Baba yetu mzazi aende kituo kidogo cha Mabasi cha pale kijijini kwetu kumsubiri mgeni akijua kuwa kwamba atakua kachukua gari jingine na muda mfupi atampokea mwanae. Kitendo cah kufika hapo stand ndogo ndipo lilikuja gari moja na hata kabla ya kuuliza kama kweli kuna ajali imetoke pale nilipomueleza, alishtushwa na habari kutoka kwa moja wa madereva aliyesikika akisema “aliwo eajali ya TAWFIQ yatokea Kenya ngu n’omwana wa Ta Bandio Mubelwa yaba alimu” (Eti kuna ajali ya gari la TAWFIQ imetokea Kenya na inasemekana hata Mubelwa motto wa Mzee Bandio alikuwemo.
Bila ya kujua nini kiliendelea Baba aliagiza mtu kuja kutueleza kuwa ajali imetokea Kenya na sio nilipoelezwa mimi na alipanda mojawapo ya magari yaliyotoka Gulioni kupeleka mizigo ya wafanya biashara na kwenda hadi mjini katiha ofisi za Tawfiq kupata habari. Kufika pale akakuta habari ni za kweli lakini jina la Mwanae halipo katika pande zote tatu yaani, wazima, majeruhi wala Waliofariki. Kuuliza namba za gari kwa wakina dada akatajiwa zile zile za gari lililopata ajali.
Kiukweli waweza pata picha ni vipi alikua akihangaika, ila kumbe jina lilikuwepo kati ya wale majeruhi sema tatizo lilikua ni jinsi gani alilitamka kutokana na kupata jeraha la ulimi.
Ilikua ni stori ambayo kiukweli ilihuzunisha sana hasa familia baada ya kupewa hizo habari lakini tulishukuru Mungu kumwona yu mzima japo alikua na majeraha yenye maumivu yaliyotokana na ajali. Nakumbuka tulipopelekwa (mimi na pacha wangu) kumwona kiukweli wote tuliishia kukumbatiana na kulia jambo lililowafanya hata wazazi kulia huku wakituachanisha. Alitueleza Mengi kuhusiana na safari hata kutupa salamu kutoka Dar es salaam. Sasa ni miaka kumi na moja tokea ajali kutokea, tuna mengi ya kumshukuru Mungu kwa kumnusuru kaka yetu kwani tumeweza jifunza mengi kupitia yeye na hasa kupitia BLOG yake ya www.changamotoyetu.blogspot.com
Kwako kaka hatuna budi kuikumbuka siku hii na twamshukuru Mungu kwa kukunusuru katika ajali hiyo. “U MEAN ALOT TO US AND WE REAL APPRECIATE YOU” sijui ni kwa jinsi gani naweza eleza umuhimu wako kwetu kama familia na hata rafiki kupitia msaada wako wa halii.akili na mali kupitia blog na hata njia nyingine kwani najua umetufunza wengi na bado naamini kuna mengi ya kujifunza kutoka kwako.
Tuikumbukapo  siku hii nipende kukuhakikishia kuwa sisi kama Familia WE ARE PROUD TO HAVE SUCH KIND OF BROTHER AND WE ARE ALL PRAYING FOR YOU.

TWAKUPENDA SANA KAKA MUBELWA NA MUNGU AKUBARIKI WEWE NA FAMILIA YAKO.


BLESSED FAMILY OF MR SIMON BANDIO.