Thursday 13 October 2011

HIVI NDIVYO SIKU YA PAULINA ILIKUWA

Mambo yakaanza hivi.
Tukiwa twamalizia siku hii ya leo siku iliyokuwa "maalyumu" kwa ajili ya kukumbuka kuzaliwa kwa mtoto Paulina Arriana Bandio nipende kutoa shukrani kwa woote mlioshiriki nasi kwa namna moja ama nyingine kuiwezesha siku hii kufana kwa kiasi ilichofana.
Hongera Saana Mjukuu wetu. We are so Proud of You.
Hakika imefana hasa kwa sababu ameweza sherehekea sherehe hii akiwa na Mama, Babu, Bibi na Baba wadogo zake (Kakulu na Kato) Na pia kuweza jumuika na baadhi ya watoto wenzake katika sherehe hii.
Twaamini hii itakuwa kumbukumbu nzuri sana sio leo tu bali maishani mwake mwoote. Nasi twazidi muombea Baraka nyingi, Hekima, Upendo na Moyo wa huruma bila ya kusahau kumcha Mwenyezi Mungu aliye Muweza wa yoote.
Matukio mengine kwa ufupi ni kama yaonekanavyo hapo chini;
Wa kwanza nilishazima sasa ni zamu ya huu tena,
Hayaaaaaaa. Nazimaaaaa.
Wooow! I thank God I have made it, 
This is a special Cake for you BABU.
Asanteeeeee na Hongera sana mjukuu wa Jina.
This is for You Mummy. I love you so much.

Na hawa ndio Maswahiba wangu huku.
Asanteni nyote kwa kuwa nasi kwa namna moja ama nyingine katika kuadhimisha kumbukumbu ya kuzaliwa mtoto Paulina.
BARIKIWA.

HAPPY BIRTHDAY SUPER PAULINA.


The Little Angle (Napenda sana kumuita MAMA)
Ni jambo la pekee kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kukulinda hadi leo hii uadhimishapo miaka miwili tangu kuzaliwa kwako. Hakika ni safari ndefu ila twamshukuru Mwenyezi Mungu kwa ulinzi wake na hata kuweza fikia hapa.

Pia nitumie fursa hii kipekee kuwakaribisha sana Nyumbani Bukoba Tanzania Wewe (PAU) na Mama Pia.
Mama na Mwana. Karibuni Sana Bukoba wapendwa.
Twafurahi sana kujumuika nanyi katika sherehe hii na kuwa nanyi katika kipindi chote tutachobahatika kuwa nanyi.
 Hakika ni furaha sana kwetu sisi kama Familia na hata kwa kila mmoja wetu kwanza Kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwalinda safarini mpaka kuwafikisha salama na pia kuwashukuru ninyi kwa kujitoa kwenu kwa hali na mali hadi kufikia Azma yenu ya kufika huku. Ujio wenu ni ishara tosha ya upendo wenu kwetu na si twaahidi kushirikiana nanyi katika kipindi chote tutachokuwa nanyi.
The Super Parents with their Angel P.A.B
Hivyo basi twawapenda na kuwaombea muwe na Afya tele na amani kwa kipindi chote tutakachokuwa nanyi huku tukimwombea pia kaka yetu Mubelwa (Baba Pau) azidishiwe afya njema na Baraka kwa kipindi choote tutakachokuwa nanyi na hata baada ya Hapo.

KARIBUNI SANA TANZANIA,

KARIBUNI SANA BUKOBA  MAMA PAULINA  NA PAULINA. 

Na mwisho niseme
HAPPY BIRTHDAY Pauliana Arianna Bandio. 

BARAKA KWENU NYOOTE.