Thursday, 10 February 2011

HIZI NI POLI-TRICKS.



Kaka yangu Mkubwa Mubelwa katika Blog yake anasegment  yake iitwayo "TANZANIA YANGU". Kiukweli naipenda sana na hujifunza na kucheka sana nionapo mambo ya kipuuzi yanayofanywa na Nchi yetu hasa kule BUNGENI. Siamini kama mambo serious yanaweza kujadiliwa kimasihara hivi ikiwa wabunge wamechaguliwa kuwawakilisha wanchi wa majimboni kwao.
Nilipokua nawaza kuandika kuhusu hilinakapata wazo kuwa ningesema TANZANIA YANGU INAYOMKANDA MBWA KIZAZI. Kwa nini nasema hivi? Wote twakumbuka dhahiri kuwa wakati Bunge likizinduliwa rasmi baada ya uchaguzi mkuu uliompatia ushindi Ndugu Jakaya M. Kikwete kuendelea kuongoza nchi kwa awamu ya pili na ya mwisho, Wabunge wa kambi kuu ya upinzani Bungeni (CHADEMA) walisusia kikao hicho na kuamua kutoka nje ya Bunge. Mengi yalisemwa na kuanza kusahaulika kama ilivyo kawaida ya Watanzania kusahau mapema ila kilichonisukuma hadi kuweka mawazo yangu kijiweni ni hali ya kushangaza ya Wabunge hao kukaa na kukubaliana na Hotuba ya Mh. Rais ilhali waliamua kutoka na kutoisikiliza. Kiukweli haikuniingia akilini na ndipo nikaanza amini kuwa Siasa sio mcheza mchafu ila wachezaji ndio wachafu. Kwa nini wawe wanafiki kiasi hicho sasa kama walijua watakuja kula matapishi yao? Na sasa nimegundua mbinu yao ya kugomea vikao na kutoka nje kisa wametofautiana kwa hoja na upinzani wenzao ama Chama tawala. Swali kwa hawa ndugu ni kwamba wanadhani kususa vikao na kutoka nje ni suluhisho la matatizo yao? Na wanawaza nini wakirudi majimboni na kuulizwa jinsi fani wamewawakilisha wananchi wao watajibu vp? Kwamba ni kwa kutoka kwenye vikao? Ila haya yote nayaona kama matokeo ya kuburuzwa kwa wanachama (wabunge) na Viongozi wa chama waliopo mjengoni na kuhamasisha migomo katika kutaka vuruga Amani wakijua wana watu wa kuwa support kutoka vyuoni. Na kama ndio njia za kushinikiza mabadiliko ya katiba kuwa ya haraka kama wanavyotaka naweza sema wataishia angukia pua kama tulivyoona vyama vya upinzani vilivyowahi kuleta upinzani kabla yao.

Tuesday, 1 February 2011

SHULE ZA KATA

Picha kwa hisani ya Kaka FRANCIS GODWI












Ikiwa ni muda mchache umepita tokea matokeo ya shule za sekondari kutangazwa, twaweza pata picha halisi ya elimu bora iliyoahidi Serikali Tukufu. Siwezi sema moja kwa moja kuwa hii ndio kudhihirisha usemi wa "MWANZO MGUMU" maana huu nauona kuwa mwanzo wa mwisho. Serikali baada ya kujenga majengo wakishirikisha baadhi ya wananchi alifanikiwa kayajenga katika kila kata kama mpango maalumu wa kuendeleza elimu Tanzania na kupata sifa kedekede kutoka kwa wafadhili wake kama UNESCO. Kwa kiwango kikubwa japo bila ya kusikiliza ni nini wananchi wake wanataka, Serikali imekua ikijichukulia maamuzi na kuendelea kuwakumbatia hao iwaitao wafadhili na kusahau kuwa "MTEGEMEA CHA NDUGUYE, HUFA MASIKINI."Kiukweli tunashindwa fanya maendeleo yetu kwa kuwa twadhani hao tunaowakumbatia NDIO WENYE MAJIBU SAHIHI YA MATATIZO YETU na kuwa wanania njema nasi lakini mimi nazidi amini bila sisi kujikana hatufiki kokote. Tuachane na Hayo, Takribani miaka minne iliyopita, Shule nyingi za kata al maarufu kama YEBOYEBO zilifunguliwa kwa nia Nzuri tu ya kutoa elimu kwa Watanzania ila sasa matokeo yametoka ni AIBU. hii ni kwa kuwa serikali ilijiandaa kutengeneza majengo wakidhani ndio maana halisi ya Shule, mengi ya majengo hayo hayakuwa na vifaa vya kufundishia wala waalimu hali iliyowalazimu hata wale walioteuliwa kwenda kwenye hizo shule kugoma. Sijui ila nipende tu pia naweza sema hili ya kuwa udhaifu ulioonekana ndio nahisi ulitumiwa na serikali kufuta Mitahani ya Kidato cha pili ilhali hawa waliomaliza wakiwa kidato cha pili  (Form two) ili kutoyaibua hayamapema ile na serikali kuoekana kushindwa kusudio lake hivyo kuamua kuwapitisha kiholela ili yanapokuja tokea yaliyotokea wao watakuwa madarakani tena na kwa hilo wamefanikiwa. Ila hofu yangu kubwa ni kwamba tuliwapitisha kiholela na kidogo wamejua "How are you," Je? s\Si hawa ndio wataongoza mapinduzi ya kisiasa miaka ijayo ama ndo kama CULTURE ya Mtanzania kusahau? Sitaki waza kwa niaba ya wengine kuhusu hili ila tu  nilikua nataka toa angalizo kuwa "MPANGO WA SASA NI KUJENGA ZAHANATI ZA KATA, JE? NA ZENYEWE SI ZITAUA KAMA SHULE ZA KATA ZILIVYOFELISHA?

TUONANE MUNGU AKIPENDA.

Sunday, 9 January 2011

HAPPY BIRTHDATE DADA AJUNA.



Malkia wa familia from Left Dada Ajuna, Mama na Dada Ninsiima.

God gave a gift to the world when you were born—
a person who loves, who cares,
who sees a person’s need and fills it,
who encourages and lifts people up,
who spends energy on others
rather than herself,
someone who touches each life she enters,
and makes a difference in the world,
because ripples of kindness flow outward
as each person you have touched, touches others.
Your birthday deserves to be a national holiday,
because you are a special treasure
for all that you’ve done.
May the love you have shown to others
return to you, multiplied.
I wish you the happiest of birthdays,
and many, many more,
so that others have time to appreciate you
as much as I do.


Instead of counting candles,
Or tallying the years,
Contemplate your blessings now,
As your birthday nears.


Consider special people
Who love you, and who care,
And others who’ve enriched your life
Just by being there.


Think about the memories
Passing years can never mar,
Experiences great and small
That have made you who you are.


Another year is a happy gift,
So cut your cake, and say,
"Instead of counting birthdays,
I count blessings every day!"

Happy Birthdate Dada Ajuna
WE LOVE TOU OUR DEAR SISTER.

Wednesday, 5 January 2011

HAPPY BIRTHDATE SWEET DADY.




Kwanza namshukuru Maanani kwa kuweza kutuvusha mwaka uliopita na kutufikisha mwaka huu wa 2011. Ni mengi sana tumepitia ambayo si kwa uweza wetu bali ni kwa nguvu zake tumewaza uona mwaka huu.

Pia nipende kumshukuru Mungu kwa kunipa wazazi hawa na hapa nianDikapo napenda  kukupongeza sana Baba kwa kukumbuka siku yako ya kuzaliwa.

Sisi kama wanao twajivunia sana kuwa nawe na Mama, umetufunza mengi ambayo sasa twaonekana kuwa kioo katika jamii na hata yanayotufanya kuishi vizuri na wenzetu ilhali tukiendeleza ule "UPENDOmlioturithisha. Twajivunia kuwa na Wazazi kama nyinyi na twawaombea Baraka zaidi na maisha marefu ili muwezeona nini matunda ya malezi meme kwa wanenu katika yale mliowafundisha. WE WILL ALWAYS BE PROUD OF YOU  na kwa pamoja twakutakia heri na fanaka katika kuikumbuka siku yako hii ya kuzaliwa.


“It is a wise father who knows his own child.” 
                      William Shakespeare.

SWEET DADY.

HAPPY BIRTHDATE BABA.

Wednesday, 22 December 2010

NIIKUMBUKAVYO MIMI DESEMBA 23, 1999.

Picha ya ajali

Ikiwa mida ya saa kumi na moja jioni, tukiwa nyumbani kijijini (NYAKIBALE) Baba aliniita na kunituma kwa Baba mkubwa katika kijiji cha jirani. Nikiwa huko mala nikapata tetesi kuwa kaka yetu mkubwa Mubelwa T, aliyekuwa safarini kutokea Dar kuja nyumbani Bukoba kapata ajali. Katika kupeleka ujumbe kwa Baba pia nikajikuta nikilieleza hili ndipo kuulizwa  kapatia wapi hiyo ajali na kusema sijasikia ni wapi kwani sikulichukulia suala la ajali kama jambo zito kutokana labda na kutokujua ajali ilikua ni nini kwa wakati huo. Nikaagizwa tena kwenda uliza hiyo ajali imetokea wapi?
Nilienda mbio bila kujali kama ni kweli ila nikihisi ni ile hali ya undugu ndio ilikua ikinisukuma kufanya yale yote na nilipofika nikaelezwa kuwa imetokea maeneo yaitwayo IGOMBE takribani kama kilometa 30 kutoka nyumbani tulipokuwa.
Ikumbukwe kwamba hiki kilikua ni kipindi cha maandalizi ya sikukuu za Krisimas na Mwaka mpya hivyo kila jambo lililohusiana na ajali hata leo huwa haliombewi ili ndugu, jamaa, wapenzi na hata wazazi wetu wasafiri na kufika na kusherehekea salama kwa pamoja huku wakifurahi, hivyo kupeleka taarifa ile ilileta hisia sana kwa wote hasa wazazi waliojua kabisa maneno yaliyosemwa na mototo kama mimi (kwa kipindi hicho) hayakua ya kujitungia.
Ilibidi Baba yetu mzazi aende kituo kidogo cha Mabasi cha pale kijijini kwetu kumsubiri mgeni akijua kuwa kwamba atakua kachukua gari jingine na muda mfupi atampokea mwanae. Kitendo cah kufika hapo stand ndogo ndipo lilikuja gari moja na hata kabla ya kuuliza kama kweli kuna ajali imetoke pale nilipomueleza, alishtushwa na habari kutoka kwa moja wa madereva aliyesikika akisema “aliwo eajali ya TAWFIQ yatokea Kenya ngu n’omwana wa Ta Bandio Mubelwa yaba alimu” (Eti kuna ajali ya gari la TAWFIQ imetokea Kenya na inasemekana hata Mubelwa motto wa Mzee Bandio alikuwemo.
Bila ya kujua nini kiliendelea Baba aliagiza mtu kuja kutueleza kuwa ajali imetokea Kenya na sio nilipoelezwa mimi na alipanda mojawapo ya magari yaliyotoka Gulioni kupeleka mizigo ya wafanya biashara na kwenda hadi mjini katiha ofisi za Tawfiq kupata habari. Kufika pale akakuta habari ni za kweli lakini jina la Mwanae halipo katika pande zote tatu yaani, wazima, majeruhi wala Waliofariki. Kuuliza namba za gari kwa wakina dada akatajiwa zile zile za gari lililopata ajali.
Kiukweli waweza pata picha ni vipi alikua akihangaika, ila kumbe jina lilikuwepo kati ya wale majeruhi sema tatizo lilikua ni jinsi gani alilitamka kutokana na kupata jeraha la ulimi.
Ilikua ni stori ambayo kiukweli ilihuzunisha sana hasa familia baada ya kupewa hizo habari lakini tulishukuru Mungu kumwona yu mzima japo alikua na majeraha yenye maumivu yaliyotokana na ajali. Nakumbuka tulipopelekwa (mimi na pacha wangu) kumwona kiukweli wote tuliishia kukumbatiana na kulia jambo lililowafanya hata wazazi kulia huku wakituachanisha. Alitueleza Mengi kuhusiana na safari hata kutupa salamu kutoka Dar es salaam. Sasa ni miaka kumi na moja tokea ajali kutokea, tuna mengi ya kumshukuru Mungu kwa kumnusuru kaka yetu kwani tumeweza jifunza mengi kupitia yeye na hasa kupitia BLOG yake ya www.changamotoyetu.blogspot.com
Kwako kaka hatuna budi kuikumbuka siku hii na twamshukuru Mungu kwa kukunusuru katika ajali hiyo. “U MEAN ALOT TO US AND WE REAL APPRECIATE YOU” sijui ni kwa jinsi gani naweza eleza umuhimu wako kwetu kama familia na hata rafiki kupitia msaada wako wa halii.akili na mali kupitia blog na hata njia nyingine kwani najua umetufunza wengi na bado naamini kuna mengi ya kujifunza kutoka kwako.
Tuikumbukapo  siku hii nipende kukuhakikishia kuwa sisi kama Familia WE ARE PROUD TO HAVE SUCH KIND OF BROTHER AND WE ARE ALL PRAYING FOR YOU.

TWAKUPENDA SANA KAKA MUBELWA NA MUNGU AKUBARIKI WEWE NA FAMILIA YAKO.


BLESSED FAMILY OF MR SIMON BANDIO.