Friday 11 February 2011

HAPPY BIRTHDATE BEST FRIEND RACHEL.



Rachel enzi Hizo.
Sijui ni lipi naweza kusema kueleza faraja niliyonayo kwa kufahamiana nawe. Najivunia mengi toka kwako. Kuanzia ukweli wa uwezo wako.Kuna kumbukumbu nyiingi maishani ambazo kwa wengine zaanza, na wengine zaendelea. Na hiyo ni sehemu ya siku yoyote ambayo kwa wengine ni "special"
Na leo ni siku muhimu kwa mmoja wa rafiki zangu aitwaye Rachel ambaye leo anatimiza mzunguko kamili wa mwaka maishani mwake. Ni "mwaka mpya" wa maisha yake na kama mmoja wa Best Friends , napenda kuungana naye katika siku hii muhimu kwake.
Akikumbuka moja ya siku yake ya kuzaliwa Udogoni.



Labda kwa kuwa nina tu-miaka kadhaa twa kukabiliana na maisha, nikuase kuwa maisha ya sasa ni ya kukabiliana na kile chema uaminicho. Kwa sasa wapo wengi ambao watajitahidi kuja na "wazo" hili ama lile kukufanya uamini kuwa HUWEZI KUFANYA UTAKALO NA KUWA UPENDAVYO.
Sikukuu ya kuzaliwa mwaka 2009.


Katika siku hii maalum kwako, nakutakia kila lililo jema katika miaka ijayo, nakupenda, nakuheshimu na nakuombea mafanikio.



HAPPY BIRTH DATE MAMA.

Thursday 10 February 2011

HIZI NI POLI-TRICKS.



Kaka yangu Mkubwa Mubelwa katika Blog yake anasegment  yake iitwayo "TANZANIA YANGU". Kiukweli naipenda sana na hujifunza na kucheka sana nionapo mambo ya kipuuzi yanayofanywa na Nchi yetu hasa kule BUNGENI. Siamini kama mambo serious yanaweza kujadiliwa kimasihara hivi ikiwa wabunge wamechaguliwa kuwawakilisha wanchi wa majimboni kwao.
Nilipokua nawaza kuandika kuhusu hilinakapata wazo kuwa ningesema TANZANIA YANGU INAYOMKANDA MBWA KIZAZI. Kwa nini nasema hivi? Wote twakumbuka dhahiri kuwa wakati Bunge likizinduliwa rasmi baada ya uchaguzi mkuu uliompatia ushindi Ndugu Jakaya M. Kikwete kuendelea kuongoza nchi kwa awamu ya pili na ya mwisho, Wabunge wa kambi kuu ya upinzani Bungeni (CHADEMA) walisusia kikao hicho na kuamua kutoka nje ya Bunge. Mengi yalisemwa na kuanza kusahaulika kama ilivyo kawaida ya Watanzania kusahau mapema ila kilichonisukuma hadi kuweka mawazo yangu kijiweni ni hali ya kushangaza ya Wabunge hao kukaa na kukubaliana na Hotuba ya Mh. Rais ilhali waliamua kutoka na kutoisikiliza. Kiukweli haikuniingia akilini na ndipo nikaanza amini kuwa Siasa sio mcheza mchafu ila wachezaji ndio wachafu. Kwa nini wawe wanafiki kiasi hicho sasa kama walijua watakuja kula matapishi yao? Na sasa nimegundua mbinu yao ya kugomea vikao na kutoka nje kisa wametofautiana kwa hoja na upinzani wenzao ama Chama tawala. Swali kwa hawa ndugu ni kwamba wanadhani kususa vikao na kutoka nje ni suluhisho la matatizo yao? Na wanawaza nini wakirudi majimboni na kuulizwa jinsi fani wamewawakilisha wananchi wao watajibu vp? Kwamba ni kwa kutoka kwenye vikao? Ila haya yote nayaona kama matokeo ya kuburuzwa kwa wanachama (wabunge) na Viongozi wa chama waliopo mjengoni na kuhamasisha migomo katika kutaka vuruga Amani wakijua wana watu wa kuwa support kutoka vyuoni. Na kama ndio njia za kushinikiza mabadiliko ya katiba kuwa ya haraka kama wanavyotaka naweza sema wataishia angukia pua kama tulivyoona vyama vya upinzani vilivyowahi kuleta upinzani kabla yao.

Tuesday 1 February 2011

SHULE ZA KATA

Picha kwa hisani ya Kaka FRANCIS GODWI












Ikiwa ni muda mchache umepita tokea matokeo ya shule za sekondari kutangazwa, twaweza pata picha halisi ya elimu bora iliyoahidi Serikali Tukufu. Siwezi sema moja kwa moja kuwa hii ndio kudhihirisha usemi wa "MWANZO MGUMU" maana huu nauona kuwa mwanzo wa mwisho. Serikali baada ya kujenga majengo wakishirikisha baadhi ya wananchi alifanikiwa kayajenga katika kila kata kama mpango maalumu wa kuendeleza elimu Tanzania na kupata sifa kedekede kutoka kwa wafadhili wake kama UNESCO. Kwa kiwango kikubwa japo bila ya kusikiliza ni nini wananchi wake wanataka, Serikali imekua ikijichukulia maamuzi na kuendelea kuwakumbatia hao iwaitao wafadhili na kusahau kuwa "MTEGEMEA CHA NDUGUYE, HUFA MASIKINI."Kiukweli tunashindwa fanya maendeleo yetu kwa kuwa twadhani hao tunaowakumbatia NDIO WENYE MAJIBU SAHIHI YA MATATIZO YETU na kuwa wanania njema nasi lakini mimi nazidi amini bila sisi kujikana hatufiki kokote. Tuachane na Hayo, Takribani miaka minne iliyopita, Shule nyingi za kata al maarufu kama YEBOYEBO zilifunguliwa kwa nia Nzuri tu ya kutoa elimu kwa Watanzania ila sasa matokeo yametoka ni AIBU. hii ni kwa kuwa serikali ilijiandaa kutengeneza majengo wakidhani ndio maana halisi ya Shule, mengi ya majengo hayo hayakuwa na vifaa vya kufundishia wala waalimu hali iliyowalazimu hata wale walioteuliwa kwenda kwenye hizo shule kugoma. Sijui ila nipende tu pia naweza sema hili ya kuwa udhaifu ulioonekana ndio nahisi ulitumiwa na serikali kufuta Mitahani ya Kidato cha pili ilhali hawa waliomaliza wakiwa kidato cha pili  (Form two) ili kutoyaibua hayamapema ile na serikali kuoekana kushindwa kusudio lake hivyo kuamua kuwapitisha kiholela ili yanapokuja tokea yaliyotokea wao watakuwa madarakani tena na kwa hilo wamefanikiwa. Ila hofu yangu kubwa ni kwamba tuliwapitisha kiholela na kidogo wamejua "How are you," Je? s\Si hawa ndio wataongoza mapinduzi ya kisiasa miaka ijayo ama ndo kama CULTURE ya Mtanzania kusahau? Sitaki waza kwa niaba ya wengine kuhusu hili ila tu  nilikua nataka toa angalizo kuwa "MPANGO WA SASA NI KUJENGA ZAHANATI ZA KATA, JE? NA ZENYEWE SI ZITAUA KAMA SHULE ZA KATA ZILIVYOFELISHA?

TUONANE MUNGU AKIPENDA.